401; Kila Kitu Kilianza Kama Wazo.

Tangu mwanzo wa kuumbwa kwa ulimwegu huu kila kitu kilianza kama wazo. Mungu alikaa akawaza kuleta uhai katika sayari ya dunia baada ya sayari hii kuwa imejaa maji pekee yake. “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu” (Mwanzo 1:26). Na hakuishia hapo vitu vingine vyote ambavyo unaviona havikutokea tu vyenyewe bali vilitokana na mawazo yake mwenyewe. Kitu […]

Ni wewe Mwenyewe Umechagua 18/11/2018.

“Mwaka 2016 tulikuwa kwenye msiba wa jirani yetu ambaye alifiwa na mama yake. Siku hiyo watu walikuwa wanalia sana na kusikitika kwa kifo kile kilichotokea. Kitu kimoja ambacho kilimshangaza kila mtu ni kwamba mtoto wa kiume wa marehemu alikuwa hana machozi na wala hana huzuni sana kama ambavyo wengi walidhani itakuwa hivyo. Watu wakajikuta wanajiuliza […]

VITU 5 UNAVYOPASWA KUVIFAHAMU ILI UWEZE KWENDA NA KASI YA MABADILIKO-9/11/2018

Tupo kwenye dunia ambayo kila kukicha kunakuwa na mabadiliko mapya katika sehemu mbalimbali hasa za kiteknolojia. Kama mwanadamu ukishindwa kwenda na kasi hii kuna mambo mengi utajikuta unashindwa kufanya au unalipa gharama kubwa sana ili tu yafanyike. Kuna vitu vingi ambavyo ungevijua vingeweza kuwa rahisi sana kwako kugundua fursa mbalimbali ambazo zingekuingizia kipato. Kwasababu hujafahamu […]

Usisubiri Hadi Ujisikie Vizuri-8/11/2018

Ni kweli hakuna kuchelewa katika mafanikio yaani hata kama una miaka 60 sasa hivi bado unaweza kuchukua hatua na kuitimiza ndoto yako. Wapo pia watu wanasema kama umepangiwa kufanikiwa utafanikiwa tu, kama umepangiwa kuwa maskini utakuwa masikini hata upambane vipi. Hayo ni aina ya mawazo ambayo unaweza kuwa nayo na yakawa sababu ya wewe kuendelea […]

Hutaondoka Ukiwa Hai -3/11/2018

Kwa vyovyote vile hata kama utaogopa kufanya mambo yaliyo makubwa, hata kama utaogopa kupoteza pesa zako bado huwezi kuondoka duniani ukiwa hai. Kama unaogopa kupata msongo wa mawazo kwasababu biashara itakusumbua Rafiki yangu hata usipoupata huo msongo wa mawazo bado hapa duniani utaondoka ukiwa umekufa. Hatujui ni kitu gani kitakuondoa duniani hivyo basi wewe endelea […]

Kufanikiwa au Kufa-2/11/2018

Kama unafikiri kutafuta pesa ni ngumu basi jaribu kukaa bila pesa uone ilivyo rahisi. Naomba nikwambie Rafiki mafanikio sio lelemama yaani sio kitu ambacho kinakuja chenyewe tu lazima uweke juhudi za kutosha. Lazima uwe na nidhamu ya kutosha. Wewe usifikiri ni kama vile ambavyo umeshajizoesha. Kuna vitu vya ziada ambavyo unatakiwa kuvifanya na hujazoea kuvifanya […]

Kufanikiwa Au Kufa 1/11/2018

Ukitaka vitu vya tofauti ni lazima ukubali kufanya vitu ambavyo hujawahi kufanya. Kama unataka kufanya vitu ambavyo hujawahi kufanya lazima ukubali kufanya maamuzi magumu ambayo hata watu wa karibu wanaokutazama wanaweza kuogopa. Kama utaendelea kubaki hivyo ulivyo na ukafanya unayoendelea kufanya kila siku maana yake utapata matokeo yale yale na hutasogea mbele hata kidogo. Wanajeshi […]

400: Hakuna AnaeKulazimisha.

Ulipokuwa mtoto kuna nyakati ulikuwa ukichelewa kuamka unakuja kuamshwa na viboko au wakati mwingine unamwagiwa maji. Kuna wakati pia ulikuwa unalazimishwa kusoma kwa bidii na unaambiwa uweke maji kwenye beseni ili usisinzie. Naomba ujiulize hivi sasa ni nani tena anaekulazamisha tena ufanye kazi kwa bidii ili uwe na pesa? Ni nani tena anaekuja kukuamsha mapema […]

399: Woga Haukusaidii Chochote Hapa..

Umekutana na mtu ukatamani sana kuzungumza nae lakini ghafla yakaanza kuja mawazo kichwani kwako kwamba, “huyu atakuwa anaringa” “mimi sistahili” “nitaongea nae siku nyingine”. Mwishoe unaondoka huku ukiwa hujaweza kuzungumza neno lolote. Huu ni woga na hofu ambayo umejitengenezea mwenyewe. Kwanza unatakiwa ujue hata kama hayo unayowaza ni ya kweli basi yeye ndie ana matatizo […]

398: Kuwa Mkweli Kwako Kwanza.

Unaweza kuwadanganya wengine lakini huwezi kujidanganya wewe mwenyewe. Ndani ya nafsi yako unajua ukweli ni upi. Ndani ya nafsi yako unajua kama Maisha unaigiza au ni kweli kile ambacho unakionesha. Mojawapo ya vitu vinavyowatesa wengi ni kujaribu kujidanganya wenyewe, unakuta unajua kabisa Matendo yako hayaashirii kabisa kile ambacho unataka lakini unajitia moyo wa uongo kwamba […]