493; USIWATHIBITISHIE. (DON’T PROVE THEM WRONG)

Kwa muda mrefu nimekuwa nikiona watu wanafanya vitu mbalimbali kama ujasirimali, biashara fulani, kazi Fulani, ili tu kuwathibitishia watu fulani waliokuwa wanawaona wao hawafai. Mfano mtu aliambiwa wewe hujawahi kuweza kitu hutaweza biashara. Anaingia kwenye biashara kwa hasira ili tu amthibitishie yule mtu kwamba anaweza. Unaweza kuambiwa wewe huwezi kupata kazi Fulani kwasababu huna elimu […]

489; Hizi Ndio Fikra Zinazokufanya Usiendelee Kwenye Maisha.

Ndani ya jiji lenye watu wengi kuliko miji mingine ndani ya Tanzania jiji la Dar es Salaam, kumekuwa na changamoto kubwa sana ya Usafiri. Hivyo basi serikali pamoja na watu binafsi wamekuwa wakiwaza kila siku ni njia gani inaweza kuwa suluhisho la tatizo hili. Katika kufikiri huko kukatokea watu wawili ambao walikerwa sana tatizo hili […]

486; Makosa Matatu Wanayofanya Wengi Baada ya Kuumizwa Kwenye Mahusiano.

Kwanza nataka ujijengee mtazamo huu kwenye akili yako, tatizo lolote linapotokea kwenye Maisha yako usiwe mwepesi sana kuona wengine ndio wanahusika, anza kuona wewe umehusikaje, imekuaje ukawa katikati ya tatizo hilo. Kuwepo katikati ya tatizo ina maanisha kuna mahali wewe ulikosea hadi ukafika hapo. Ukisalitiwa inamaanisha kuna mahali ulikosea ukajikuta uko kwenye kusalitiwa, ndio unaweza […]

483; Unapohisi Kama Mungu Amekuacha

Kumzuia mtoto asitembee mwenyewe kwasababu tu unaogopa ataanguka na ataumia sio kumsaidia ni kumlemaza.  Hivyo ndivyo ilivyo katika maisha yetu ya kila siku. Kuna vitu kama utaendelea Kuogopa kufanya au kutaka Kusaidiwa kila unapofanya unakuwa unalemaa. Lazima ujifunze kufanya mwenyewe ili uwe na Ujasiri na kujiamini. Kamwe usifikiri Mungu amekuacha wakati wa magumu anataka ujifunze […]

482; Mbegu Inayojiotea Yenyewe.

Mti unapopukutisha majani na matunda unaweza kufikiri imepoteza kitu kikubwa sana. Mfano ndege wanapokuja na kula matunda kisha yakaanguka chini yakaoza. Wewe kwa akili zako za kibinadamu unaweza kuona ni uharibifu. Lakini kwa akili za Kimungu sio uharibifu yale matunda yaliyooza hugeuka kuwa mbolea kwa mti ule ule ulioyadondosha. Kuna vitu ukivifanya kwenye Maisha ya […]

480; Tambua Kusudi La Mungu Maishani Mwako.

Unaweza kujikuta unafanya mambo hayaendi kabisa na wala huoni matokeo yake unayoyataka kwasababu  upo nje ya kusudi la Mungu. Mungu  hajakuumba kwa bahati mbaya ulikuja kwa kusudi na upo hai ili utimize kusudi. Hakikisha unalitambua kusudi la Mungu maishani mwako ili uweze kuishi maisha yenye furaha na baraka za Mungu. Hujazaliwa duniani ili uje kuzaa […]

479; Kabla Hujakata Tamaa, Jaribu Njia Nyingine.

Kuna Wakati wale uliowatarajia Wakusaidie watakugeuzia Mgongo. Usiogope, Usilaumu, Usilalamike Mtumaini Mungu, na Jaribu Njia Nyingine. Mwaka 2016 nilijitoa muhanga wa kutafuta mtaji wa kufanyia biashara. Niliingia kwenye simu yangu nikaona nina namba zisizopungua elfu moja. Katika hizo namba watu Karibu 500 walikuwa wananifahamu. Nikasema ngoja niwatumie watu hawa kukusanya mtaji. Nikaandaa ujumbe mzuri nikawatumia […]

472; Mbinu za Kuweza Kuwa na Furaha Wakati Wote.

Kuna utafiti ulifanyika wa kidunia ukaja na majibu ya nchi zinazoongoza kwa kukosa furaha duniani. Mojawapo ya nchi iliyotajwa ilikuwa ni nchi ya Tanzania, kwasababu mimi ni mtanzania sikuwa na majibu sahihi wala utafiti wa kupinga hili ila ninaweza kukuandikia wewe mambo machache ambayo unaweza kufanya na yakakuletea furaha binafsi. Watu wengi wamekuwa wanafikiri kwamba, […]

470;USHAURI: MUONDOE CHUMA ULETE HUYU KWENYE PESA ZAKO.

Mojawapo ya vitu vinavyowafanya watu waishi maisha ya magumu sana hapa duniani ni kukosa namna bora ya kupangilia na kuendesha maisha yao. Kingine ni kwamba wengi wanapenda kuishi maisha ya kuiga, kwasababu umeona jirani yako ana maisha Fulani hivi na wewe unataka uanze kuishi hivyo. Sio vibaya kutamani vitu vizuri kwenye maisha yako lakini ni […]

468; Watu Sahihi, Watu Wazuri.

Kwenye Maisha tunawahitaji watu sahihi. Watu Sahihi sio lazima wawe Wazuri kwetu wanaweza kuwa watu wabaya lakini ni sahihi. Kusudi la hao watu kwenye maisha yetu ndio litaamua usahihi wao. Unaweza kukutana na mtu anakuchukia bila sababu halafu kwa kukuchukia kwake kukawa sababu ya wewe kusonga mbele Zaidi. Kuna watu wakikupenda ndio wanakuharibu, badala ya […]