484; Ukiachwa Ni Nani Anakuwa Amepoteza?

Nilimpenda sana, nilimwonesha mapenzi yote, nilimpa kila alichokuwa anataka lakini nimeambulia kuachwa. Hayo ni mojawapo ya maneno ambayo watu wengi wamekuwa wakiyatoa baada ya kuchwa na wale waliokuwa wanawapenda sana. Nimetafakari nikajakugundua kama ni kweli ulikuwa unamfanyia mambo yote mazuri na kumpa kila alichokuwa anataka halafu akaja akakubwaga ukweli ni kwamba sio wewe uliepoteza bali […]

483; Unapohisi Kama Mungu Amekuacha

Kumzuia mtoto asitembee mwenyewe kwasababu tu unaogopa ataanguka na ataumia sio kumsaidia ni kumlemaza.  Hivyo ndivyo ilivyo katika maisha yetu ya kila siku. Kuna vitu kama utaendelea Kuogopa kufanya au kutaka Kusaidiwa kila unapofanya unakuwa unalemaa. Lazima ujifunze kufanya mwenyewe ili uwe na Ujasiri na kujiamini. Kamwe usifikiri Mungu amekuacha wakati wa magumu anataka ujifunze […]

480; Tambua Kusudi La Mungu Maishani Mwako.

Unaweza kujikuta unafanya mambo hayaendi kabisa na wala huoni matokeo yake unayoyataka kwasababu  upo nje ya kusudi la Mungu. Mungu  hajakuumba kwa bahati mbaya ulikuja kwa kusudi na upo hai ili utimize kusudi. Hakikisha unalitambua kusudi la Mungu maishani mwako ili uweze kuishi maisha yenye furaha na baraka za Mungu. Hujazaliwa duniani ili uje kuzaa […]

479; Kabla Hujakata Tamaa, Jaribu Njia Nyingine.

Kuna Wakati wale uliowatarajia Wakusaidie watakugeuzia Mgongo. Usiogope, Usilaumu, Usilalamike Mtumaini Mungu, na Jaribu Njia Nyingine. Mwaka 2016 nilijitoa muhanga wa kutafuta mtaji wa kufanyia biashara. Niliingia kwenye simu yangu nikaona nina namba zisizopungua elfu moja. Katika hizo namba watu Karibu 500 walikuwa wananifahamu. Nikasema ngoja niwatumie watu hawa kukusanya mtaji. Nikaandaa ujumbe mzuri nikawatumia […]

477; Sio Yako Hadi Pale Utakapoitoa Kichwani.

“Kuna kipindi Fulani nilisafiri kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kikazi. Nilipofikia kwenye familia moja ambayo ilikuwa inanifahamu. Sikuwa nawafahamu sana watu kwenye ile familia Zaidi ya baba mwenye familia ambaye alikuwa mwenyeji wangu. Wakati naendelea kukaa pale nilitokea kuzoeana na binti yake sana hadi nikaanza kuona hisia za upendo. Kiukweli nilikuwa namheshimu sana mzee yule […]

476; Unahitaji Watu Zaidi Kuliko Unavyohitaji Pesa.

Mtu Tajiri kuliko wote duniani kwa haraka haraka ukifikiria unaweza kudhani kilichomfanya akawa Tajiri ni pesa zake au akili zake pekee. Ila ukija kutafakari katika upande mwingine unagundua kwamba ukiwa na pesa pekee bila watu utaishia kuzitumia kwa matumizi yako binafsi. Ukiwa na akili nyingi za kugundua vitu halafu huna watu utaishia kugundua tu lakini […]

475; Huu ndio Ukosoaji Ninaoupenda.

Mwanzoni simu za smartphone zilipoanza kuja kulikuwa na tatizo kubwa la simu hizo kutokukaa na chaji. Baada ya muda sio mrefu wakaja watu wakaleta Power Bank ambayo inahifadhi chaji. Tatizo linguine likaanza kuonekana kwenye simu hizi ni vioo kupasuka mara kwa mara. Haichukua muda wakaja na Screen Protector. Yaani unanunua simu halafu unakuja tena unanunua […]

474; USHAURI: Unapofika Wakati Unaona Maisha Yako Hayana Maana wala Thamani Tena.

Nilikuwa napitia maisha ya mwandishi mashuhuri kutoka Brazil, Paulo Coelho aliendika vitabu vingi kikiwemo cha The Alchemist. Mojawapo ya jambo gumu alilowahi kupitia maishani mwake ni alipokuwa na umri wa ujana yaani miaka ya 18-20 aliwahi kupelekwa hospitali ya vichaa mara tatu na wazazi wake. Wazazi wake waliziona tabia zake na kufikiri ni mtu aliechanganyikiwa […]

472; Mbinu za Kuweza Kuwa na Furaha Wakati Wote.

Kuna utafiti ulifanyika wa kidunia ukaja na majibu ya nchi zinazoongoza kwa kukosa furaha duniani. Mojawapo ya nchi iliyotajwa ilikuwa ni nchi ya Tanzania, kwasababu mimi ni mtanzania sikuwa na majibu sahihi wala utafiti wa kupinga hili ila ninaweza kukuandikia wewe mambo machache ambayo unaweza kufanya na yakakuletea furaha binafsi. Watu wengi wamekuwa wanafikiri kwamba, […]

469; UsiishieNjiani: Sio Mhamasishaji ni Wewe.

Katika kazi yetu hii ya kushauri, kutia moyo, na kuhamasisha watu huwa tunakutana na changamoto. Mojawapo ya Changamoto kubwa ni pale mtu anapokuuliza wewe umeshafanya nini mpaka unataka kunihamasisha mimi? Yaani mtu anasema ili aweze kusikiliza kile unachomwambia na kukifanyia kazi hadi aone umefanya kitu fulani. Labda tayari una gari, au una maisha fulani hivi […]