Unaweza ukashangaa sana kumkuta mama anawafurahia Watoto wa wengine na kucheka nao vizuri sana lakini wakati huo huo anamchukia sana mtoto alieko nyumbani kwasababu ni mtoto wa nje. Ulishawahi kukutana na mtu anakuchukia tu kwasababu wewe umefikia hatua Fulani ambayo yeye hajafika utafikiri labda wewe ndio sababu ya yeye kutokufika hapo.

Ni ajabu sana kwenye jamii zetu tuna watu wana tabia hizi za ajabu za chuki zisizo na maana yeyote. Chuki hizi zinasababisha mtu anaanza kupanga na kutenda mabaya juu ya wengine ambao hawana hata sababu na Maisha yao. Sasa Rafiki yangu kabla hatujaendelea embu jiulize kuna mtu yupo ndani ya moyo wako unamchukia tu bila ya sababu? Eti unafikiri kuna kitu kama hicho kumchukia mtu bila sababu? Kwanini sasa usimpende bila ya sababu?

Maisha haya ili tuweze kuyafurahia vyema ni kwa kuoneshana upendo, chuki ndio zinayafanya Maisha yawe magumu Zaidi. Chuki ndio zinaondoa amani kwenye dunia yetu. Ni ujinga sana kujifanya unampenda mtoto wa jirani halafu pale nyumbani kwenu kuna mtoto unamchukia kisa tu sio wa ukoo wenu, aliletwa kuja kuishi hapo.

Ni unafiki uliopitiliza kujifanya unaipenda ndoa ya watu Fulani hivi ambao hamna uhusiano wa damu halafu hapo kwenu unamchukia yule wifi yako au shemeji yako bila ya sababu tu. Huo ni ujinga au mimi naweza kuuita ni utoto yaani ni kwamba kuna sehemu kwenye akili yako bado haijakua bado una utoto ndani ya akili yako bila kujalisha una miaka mingapi.

Embu Rafiki yangu achana na hizi chuki za ajabu ajabu, hazina maana. Hizi ndio zinasababishaga watu waendeane kwa waganga na wengine kuwekeana sum utu. Ni ujinga mtu tena ujinga wa kiwango cha juu kusema humpendi mtu bila ya sababu. Tena unakuta mtu anasema yaani huyo naona damu zetu hazijaendana kabisa. Yaani wewe una matatizo kabisa, damu hazijaendana ndio nini. Wewe una tabia za kichawi hizo embu ziache, anza kuwapenda watu bila ya sababu. Mtu hajakufanyia chochote unamchukia tu bila ya sababu ili iweje sasa.

Kama wewe unamjua mtu mwenye chuki za aina hii embu mtumie asome apate uponyaji. Hayo ni mapepo, na ukiendekeza hautaenda mbinguni, yaani chuki ni sawa na uuaji. Kuua mtu huanza kwa kumchukia.

Nikutakie kila la kheri

Rafiki Yako Jacob Mushi.

Hii ya Kuchukia kijinga naomba uishie Njiani usiendelee nayo sawa.

www.jacobmushi.com/coach

2 Responses

  1. Aiseee had me wakati mwingine huwa nashangaa San
    Lakini naamin ujumbe utakuwa umefik
    Thanks a lot

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading