Ni wewe utawajibika pale unapoingia kwenye matatizo bila kujali ni nani aliyeyasababisha.

Ni wewe utatakiwa kuchukua hatua pale mambo yanapokuwa magumu kwasababu ya uzembe unaoufanya sasa.

Ni wewe utakalipa gharama za ulaji mbovu unaokula sasa pale utakapoanza kusumbuliwa na magonjwa.

Ni wewe utakaelipa gharama ya ujinga unaoundekeza sasa hivi, unaambiwa ujifunze hutaki,

Unaambiwa uweke akiba unapuuza kwasababu sasa hivi unapata kila unachokitaka.

Unaambiwa ujenge tabia za mafanikio hutaki, unaona wewe hakuna wa kukuelekeza kwasababu tayari unakila unachotaka.

Ni wewe utakaewajibika kwa lolote litakalotokea kwenye maisha yako kutokana na uzembe au kwa namna yoyote ile.

Wale uliokuwa unawaona hawana maana wakati wakikushauri watakutoza fedha ukiwarudia kwenda kuwaomba ushauri tena.

Wale uliokuwa unaona kama wanafuatilia maisha yako, hawajielewi, wenyewe hawana maisha kama yako kwa hivyo hawawezi kukushauri chochote utawafata kwa gharama kubwa.

Sikutishi nakwambia ukweli, ile gharama unayokwepa kulipa sasa hivi utakuja kuilipa siku moja huko mbeleni, bahati mbaya sana utailipa na riba.

Kama unaona ni ngumu sana sasa hivi kuweka akiba kwasababu pesa zipo za kutosha ipo siku utaingia gharama ya kukopa mambo yakiwa mabaya.

Ni wewe ndiye utakaewajibika kwa makosa yako, sisi tutaendelea kubaki kama washauri tu.

Ni muhimu kuchukua hatua sasa kwasababu hata ukikwepa lazima utakuja kulipia gharama kwa kile ulichokikwepa.

Nakutakia Kila La Kheri.

Kupata huduma na Bidhaa mbalimbali kwenye mtandao huu bonyeza linki hii www.jacobmushi.com/kocha

Makala hii imeandikwa na Kocha Jacob Mushi. Mwandishi wa Vitabu na Makala, Kocha wa Maisha, na Mjasiriamali.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading