Nukuu za Maisha (Malengo, Mafanikio, Mahusiano n.k) ni Kitabu kinachokupa muongozo wa maneno ya kutafakari kila siku asubuhi ili uweze kuwa na siku bora na yenye mafanikio.

Kitabu hiki kina nukuu 400+ ambazo zinakupa uwezo wa kufikiri vizuri, kuishi kwa furaha na kuweza kusonga mbele katika kile unachokifanya.

Nukuu za Maisha ni mjumuisho wa nukuu za furaha, nukuu za mahusiano, nukuu za upendo, falsafa za maisha, nukuu za mafanikio, nukuu za biashara, nukuu za hamasa, nukuu za malengo, nukuu za kutia moyo, nukuu za kuongeza ujasiri, nukuu za kuongeza kujiamini na kadhalalika usiache kusoma kitabu hiki.

NUKUU ZA MAISHA ni mkusanyiko wa nukuu ninazoandika kwenye mtandao wa Instagram kila siku. Nimezikusanya zaidi ya 400 na utaweza kuzisoma kwenye kitabu kimoja.

SHUHUDA ZA NUKUU HIZI KWENYE MAISHA YA WATU

Hakika nimesoma maandiko yako mengi sana nimepata mafanikio makubwa sana kifikira sasa nimeweza kukaribia malengo niliyojiwekea Mungu akutie nguvu. Pia baada ya kumaliza kusoma kitabu cha USIISHIE NJIANI nimejifunza mambo mengi sana.

EvaStella Ricknelson

Tangu nimeanza kufuatilia NUKUU za Jacob kwenye mitandao ya kijamii nimeona mabadiliko makubwa, nimekuwa jasili, najiamini, napambana sana kwenye utafutaji wangu, na nimejifunza kuto kukata Tamaa.

– Stella Samwel

 Katika nakala zako na jumbe zako zimenifungua macho maana Nilikuwa sioni wapi ninapokwenda katika maisha yangu yapo Mambo mengine niliyaona hayawezekani lakini leo nayaona yanawezekana.

Elisha Dismas

Ni kweli nimepata vitu vingi toka kwenye nukuu zako za Maisha! Ukweli ni kwamba maisha halisi ni Maarifa, uko vizuri, zidi kutafuta maarifa utaishi ndoto zako pia ukimtanguliza Mungu mbele maana Zawadi na vitu vingine vyote vyatoka kwa MUNGU

Justin Kabembo

 “Tangu nimeanza kufuatilia NUKUU za Jacob kwenye mitandao nimeona mabadiliko makubwa kwenye Maisha yangu. Kwanza nimeamini maisha ni kuthubutu. Pili kila jambo linaanzakufanikiwa katika akili yako. Tatu, Matendo yako yanakuwezesha kutengeneza ile picha uloifikiria kuwa halisi. Nne, rafiki/mchumba/mke/mume ni chachu ya mafanikio au changamoto za mafanikio yako. Hivyo chagua maisha!!

Joshua S. Lebabu

Tangu nimeanza kufuatilia Makala zako nimekuwa nikipata maneno mazuri ya faraja ya kutokukata tamaa katika safari ya mafanikio

Prosper Cosmas

Tangu nimeanza kusoma nukuu na vitabu vya jacob Mushi. Nimepata mwanga mkubwa sana nimekuwa mtu mwenye upeo na maono makubwa kimafanikio, japo ni katikati lakini angalau nimekuwa mfano wa kuigwa. Isitoshe Jacob amenishauri mambo mengi ya kimaisha na kibiashara. Ni miongoni mwa waandishi bora hapa nchini. Hakika huwezi Jutia ukisoma nukuu na vitabu vyake.

Denis Tesha

Tangu mwaka 2016 nilipoanza kukufuatilia umenifanya niwe mtu mpya Na niweze kufanya mambo ambayo sikutegemea kuwa yanafanyika.

Baraka MWAMPULULE

“Kwakweli nukuu zako zinatoa mwanga mpya na kutia moyo kwa walioanguka wainuke na kuendelea.”

Mtaalam Md

Kwanza kabisa namshukuru Mungu kukuleta maishani kwangu Kaka, hakika umekua sehemu ya mabadiliko katika nyanja tofauti tofauti maishani mwangu, Vitu vingi Sana nimejifunza na ninazidi kujifunza kutoka kwako, umenifundisha ujasiri wa kuthubutu, umenifundisha namna ya kuyatumia matatizo Kama fursa ya kuingiza kipato, namna ya kuishi na watu, ni  mambo mengi sana, Hadi mda huu naona utofauti mkubwa Sana katika maisha yangu tofauti na nilivyokuwa mwanzoni, ubarikiwe Sana na uzidi katika Hilo.

Peter Mahunja.

Nimejifunza Ni jinsi gani ninaweza kujisimamia binafsi.

Kareem

Tangu nimeanza kusoma kazi zako, Vitabu na kwa blog pamoja na nukuu nimejifunza vingi vya kunipa hamasa ya kusonga mbele na zimechangia kubadilisha maisha yangu kifikra kwa kiasi kikubwa.

Peter Mbizo

Binafsi mimi makala zako zimenifanya niwe mtu wa kujiamini na kufanya kila kitu bila kukata tamaa na kuwa mtu subira maana Hapo mwanzo nilikuwa mtu wa wasiwasi na muoga wa kujaribu kufanya kitu asante sana kwa makala zako za kutia moyo.

Nelson Frank Mushi.

Hata pasipo ya kuniuliza ni mabadiliko gani nimeweza kuyapata kupitia kufuatilia nukuu hizi ningelikuambia siku moja kuwa ama hakika wewe ni nabii ulikubalika kwenu. Nukuu zako zimenijenga sana katika swala la kutokujikatia tamaaa kulingana na hali za maisha niyoyaishi kila siku ni hii ni baada ya kusoma jarada lako moja kuhusu maisha ya Daud pamoja na wazazi wake hadi kuufikia ufalme.

Steven Samwel

Nashukuru mno Bro kwa kweli Mimi ni mdau wako namba moja, mafundisho yako yanafariji na kukufanya mtu ujitambue, Kama Kuna sehemu ulisinzia basi ghafla unaamka, mie ni single mom kwa hiyo Niko na changamoto nyingi ninazopitia katika kujikwamua, Kuna muda nakuwa na stress ghafla nikikusoma naona Kama wasema Mimi, basi napata funzo na kupiga hatua nyingine.

Rehema Lebby

 

Tangu nimeanza kusoma kusoma kitabu chako nimejitambua kwa kweli nimejifunza kuwa na mimi ninaweza kufanya jambo nikaweza kwa uelewa wangu nilionao, nimejifunza ni aina gani za marafiki natakiwa kuwa nao, ni mambo gani inabidi niyafanye ili niweze kutimiza maono yangu kwa kweli hiyo ni kwa ufupi lakini nimejifunza mengi na bado naendelea kuyatendea kazi.

Nuriath Nuru

Kiukweli bila kuficha toka nianze kufuatilia nukuu zako ndugu jacob mushi kuna mabadiliko makubwa kwangu. Kwanza kwasasa, najiamini, Sina hofu, Nathubutu, Siahirishi mipango, Nimekuwa na nidhamu Asante sana kwa nukuu zako.

Wille Balisho

Nadhani kila mtu hapa Duniani anahitaji mtu wakumtia moyo, inawezekana maneno ya mtu yakatosha nikiwa nasoma najitia moyo kwa maneno yako nakusonga mbele bila kuishia njiani.

Palmaraham Nkya

NAMNA YA KUPATA KITABU HIKI:

Bei ni Tsh 10,000/= hardcopy/softcopy,

Namba za Malipo.

0654 726 668 Tigopesa. Jacob Moshi,

10 Responses

  1. Nitakutafuta kwa ajili ya kupata kitabu kaka,makala zako zinanifanya nionekane mtu mkubwa ninae weza kufanya karibu kila kitu.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading