“Kaka Jacob naomba ushauri wako, sijui hata nifanyeje, huu ni mwaka wa 5 sasa nimekuwa najaribu kuingia kwenye mahusiano tofauti tofauti lakini naambulia kuachwa na kuumizwa. Mara ya mwisho nilikutana na mkaka mmoja ambaye tulianza nae mahusiano kwa haraka na motomoto sana lakini mwisho wake nikaja kuona anaanza kupunguza mapenzi taratibu, kaanza kupunguza mawasiliano na mpaka akafikia kupotea kabisa.

Yaani niseme kwamba yaani imekuwa tabia ni hiyo tu. Wanakuja kwa kasi na baada ya muda wanaondoka kama vile hatukuwahi kujuana kabisa. Sasa mpaka nakutumia ujumbe huu nimejaribu kutafakari sana sijapata majibu. Nimejaribu kuangalia labda ni mimi mwenyewe nina matatizo, labda kuna mahali nakosea, bado sijapata majibu.

Najihisi kama mtu aliekwama kwenye tope zito na kila ninaempa mkono anivute anaishia kuniacha kwenye tope hilo. Embu nishauri kaka nifanye nini? Muda unakwenda na sijawahi kudumu kwenye mahusiano Zaidi ya miezi mitatu, wengi wanaishia mwezi mmoja mpaka wa tatu.

Nifanyeje?”

Nataka nizungumze na mtu ambaye anajihisi amekwama kwenye tope la namna mbalimbali. Inawezekana na wewe unapitia hali ambayo unajihisi umekwama kwenye tope zito na unahitaji mtu wa kuja kukutoa humo.

Mara nyingi hali mbalimbali tunazopitia kwenye Maisha yetu huwa hazihitaji watu wengine kuja kututatulia bali sisi wenyewe unakuta tunahitaji kupata utulivu mkubwa wa akili ili tuweze kuona ni wapi tunakosea tuchukue hatua. Wakati mwingine ukiwa kwenye tope na mtu akaja kwenye Maisha yako akagundua kweli upo kwenye tope ni rahisi kukukimbia kwasababu anajua akijaribu tu kukusaidia na yeye atajikuta kanasa hapo uliponasa wewe.

Wakati mwingine sio kila anaekukimbia inamaanisha wewe ndio una matatizo hapana wengi hukimbia kwasababu ya woga walionao, wanahisi watanasa kwenye mtego uliokunasa.

Vitu vya Kuzingatia:

Punguza Kasi,

Ukiwa mtu mwenye kasi kubwa sana hasa mahusiano yanapokuwa mapya ni rahisi kuchokana mapema kabla hujafika popote. Lazima ujifunze kwenda taratibu na kama mtu sio sahihi utaona tu atakukimbia kwasababu yule asie na lengo la kudumu na wewe akiona wamcheleweshea anachokitaka ataamua kuondoka. Usiruhusu mtu ayajue madhaifu yako mapema wakati hamjajenga msingi mzuri ambao unaruhusu kuwekana wazi kwa baadhi ya mambo ambayo ni siri.

Soma: Acha Kutafuta Samaki Msituni

Tumia akili yako Zaidi Kuliko Hisia,

Fanya maamuzi kwa kutumia Akili, Usiruhusu Hisia Zikuongoze.

Ukitulia Ndio Utaweza Kujua Kile Unachokitaka.

Wakati mwingine Subira Hutujulisha kama ni kweli tunavihitaji vitu Fulani au vinaweza tu kupita. Ukipanda mbegu mbichi ya mahindi ni rahisi sana kuoza kuliko kuota, kwenye Maisha yetu kuna vitu vinatakiwa vipewe Subira ili viweze kukomaa ili vifae kutumia kwenye hatua nyingine. Mara kwenye mapenzi tunawahi sana kufanya vitu ambavyo vilitakiwa vipewe muda ili vikomae kwanza. Kwasababu kama havijakomaa urahisi wa kuharibika unakuwa mkubwa.

UVUMILIVU;

Uvumilivu wahitajika sana sio kuvumilia mateso hapana nazungumzia kuvumilia hasa ule wakati unakihitaji kitu na hakipo au hakipatikani kwa wakati huo. Kuweza kudhibiti hisia zako na kusema sitaingia kwenye mahusiano kwa wakati huu ambapo nipo kwenye hisia kali za kuhitaji mtu ni jambo la muhimu sana kwasababu hisia kali zaweza kukusababishia uanzishe mahusiano na mtu asiye sahihi au ambaye hatadumu tena baada ya hisia zako kuisha.

MAOMBI;

Kumuomba Mungu ni muhimu sana kwasababu yeye atakupatia muongozo na pia atakukwepesha na wale ambao hawakutakiwa kuja kwenye Maisha yako. Mungu atakuepusha na vile vitu ambavyo havikutakiwa kutokea kwenye Maisha yako.

Nakutakia Kila la Kheri.

Rafiki Yako Jacob Mushi.

7 Responses

  1. Kimsingi ni kuomba mungu tu, sababu mahusiano mengi ya kizazi cha sasa uongo ni mwingi. N.k kama una hulka ya kijirahisi kwa mwanaume, kutegemea sana mwanaume kiuchumi, au kuonyesha kuomba ndoa kwa maneno inabidi ujifinze kuacha/kupunguza.

      1. Pole Saana wanaume wasasa wengi sio waaminifu kuwa na Subra yaani usiingie tena mahusiano tuliza akili ikiwezekana toka mazingira unayoishi tembelea ata ndugu mkoa mwingine.

Andika Maoni Yako Hapa

Discover more from Jacob Mushi

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading